Loading...

EID MUBARAK, TUZINGATIE USALAMA WA WANETU

Loading...

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala nchini Tanzania, Alhaj Zuberi Chembela amewataka wazazi kuwa makini kwa kuwalinda watoto wao wakati wakisherehekea sikukuu ya Eid-El-Adh’aa.

Amesema wazazi wana jukumu kubwa la kuhakikisha watoto wao wapo salama na hawafanyi matendo yasiyo mpendeza Mungu.

Akitoa salamu wakati wa Swala ya Eid-El-Adh’aa na Baraza la Eid kitaifa iliyofanyika kwenye viwanja vya msikiti wa Kibadeni, Chanika jijini Dar es Salaam, Kamanda Chembela amesema pamoja na ulinzi huo kwa watoto, wazazi na viongozi wanapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa kutenda matendo mema.

“Isifike mahali unamkataza mtoto kufanya jambo baya wakati wewe kiongozi na mzazi unaongoza kwa kutenda jambo baya,” amesema Kamanda Chembela

“Niwatake na niwaombe Waislamu wote msherehekee sikukuu hii kwa amani, ulinzi umeimarika na kila mahali kila kitakachotokea ambacho kitaonyesha dalili za uvunjifu wa amani kitashughulikiwa.”

Na Neema Joshua.
.

.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.

EID MUBARAK, TUZINGATIE USALAMA WA WANETU EID MUBARAK, TUZINGATIE USALAMA WA WANETU Reviewed by Distri Music on 8/12/2019 12:54:00 PM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.