Loading...

AUZA BIKIRA YAKE KWA DAU LA MILIONI 800

Binti Rosalie akiwa katika picha ya kificho
Binti aliyejulikana kwa jina la Rosalie Pinho (19) kutoka Minas Gerais huko Brazili anauza bikira yake kwa njia ya mnada ili kutengeneza pesa ili kusaidia familia yake masikini, ikiwemo kumnunulia nyumba ya kuishi mama yake mzazi.

Rosalie imeripotiwa anakubali dau la kuanzia Euro (£) 264,000 kutoka kwa 'mabwana' ambao ambao wataburidika naye kwa masaa 12.

Katika mahojiano na mtandao mmoja wa MailOnline Rosalie amesema kuwa anauza usichana wake kwa sababu familia yake inakabiliwa na matatizo makubwa ya kifedha, na hata kushinda kujihudumia chakula mara kadhaa.

Pia anasema ana matumaini ya kuvuna pesa za kutosha, na hata kuhamia mjini ili anunue nyumba kubwa kwa ajili ya kuishi mama yake na pesa nyingine kwa ajili ya kulipa ada zake za chuo.

Binti huyo mwenye umri wa miaka 19 pia anakusudia kutumia pesa hizo kuanzishia biashara, ambayo itamsaidia kuishi bila kuwa na wasi wasi wa kifedha.

Alisema: "Sikuwahi kuwa na mahusiano ya kimapenz
Loading...
na kijana yeyote kufikia kiwango cha kufanya ngono zaidi ya kupigana mabusu tu, na ndio ilikuwa mwisho wa mipaka ya mahusiano yangu. Hapo mwanzo wazo la kushiriki mapenzi na mtu nisiyemjua ilikuwa ngumu sana lakini nikaona nivyema nifanye na nivune pesa kuliko kuharibiwa usichana wangu na mtu ambaye angediriki kuuvunja moyo wangu."

Mbrazili huyo pia alidai ameshapokea dau la Euro (£) 440,000 tayari mpaka sasa.

"Haiwezi niumiza kwakuwa maneno ya watu hayawezi tatua matatizo yangu lakini mnada pekee utafanya hivyo. Tunaishi katika kipindi cha uhuru wa kujamiiana, ni mwili wangu na sheria zangu."
Rosalie akionyesha baadhi ya viungo vya mwili wake.
Orodha ya vigezo na masharti ili kushinda mnada wa bikira yake

AUZA BIKIRA YAKE KWA DAU LA MILIONI 800 AUZA BIKIRA YAKE KWA DAU LA MILIONI 800 Reviewed by By News Reporter on 1/30/2018 03:42:00 PM Rating: 5

Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.