Loading...
Polisi wa Israel wamesema wamapata ushahidi wa kutosha wa mashitaka ya rushwa na udanganyifu wa fedha kufunguliwa dhidi ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu na mke wake.
Inadaiwa kwamba Netanyahu na kampuni ya Bezeq telecom walifanya makubaliano yanye thamani ya mamilioni ya dola ili shirika la habari la Walla ambalo ni kampuni ndogo ya Bezeq liwe linachukua mtazamo chanya wakati linaporipoti taarifa zinazomhusu Netanyahu.
Netanyahu amekanusha madai dhidi yake. Iwapo atafunguliwa mashitaka, waziri huyo mkuu wa Israel anayetumikia muhula wa nne madarakani atakabiliwa na mojawapo ya changamoto kubwa zaidi kisiasa.
Uamuzi wa mwisho wa iwapo Netanyahu atafunguliwa mashitaka au la utachukuliwa na mwanasheria mkuu wa Israel ambaye bado anatafakari iwapo amshitaki kuiongozi huyo na kesi nyingine mbili zinazomkabili za madai ya hapo awali ya rushwa, udanganyifu na uvunjaji wa uaminifu.
Na George Michael.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
Inadaiwa kwamba Netanyahu na kampuni ya Bezeq telecom walifanya makubaliano yanye thamani ya mamilioni ya dola ili shirika la habari la Walla ambalo ni kampuni ndogo ya Bezeq liwe linachukua mtazamo chanya wakati linaporipoti taarifa zinazomhusu Netanyahu.
Netanyahu amekanusha madai dhidi yake. Iwapo atafunguliwa mashitaka, waziri huyo mkuu wa Israel anayetumikia muhula wa nne madarakani atakabiliwa na mojawapo ya changamoto kubwa zaidi kisiasa.
Uamuzi wa mwisho wa iwapo Netanyahu atafunguliwa mashitaka au la utachukuliwa na mwanasheria mkuu wa Israel ambaye bado anatafakari iwapo amshitaki kuiongozi huyo na kesi nyingine mbili zinazomkabili za madai ya hapo awali ya rushwa, udanganyifu na uvunjaji wa uaminifu.
Na George Michael.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
WAZIRI MKUU ISRAEL KUSHTAKIWA KWA RUSHWA
Reviewed by By News Reporter
on
12/03/2018 08:15:00 AM
Rating:

Hakuna maoni: