Loading...

MBUNGE TUNDU LISSU AVULIWA UBUNGE, SABABU HIZI HAPA

Loading...
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai amesema kuwa amemuandikia barua mwenyekiti wa NEC kumtaarifu kuwa kiti cha Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki kipo wazi, kutokana na Mbunge wa jimbo hilo, Mhe. Tundu Lissu (CHADEMA) kutokuwepo bungeni bila taarifa na kutokujaza fomu ya tamko la mali na madeni.

Akitaja sababu kubwa mbili, Spika amesema ni kutotoa taarifa rasmi ya maendeleo yake, huku akionekana sehemu mbalimbali.

Sababu ya pili ni kushindwa kujaza fomu za maadili ya viongozi za Tume ya maadili, hivyo kupoteza sifa za kuwa Mbunge.
Na Mary Mkeu.
.
.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
MBUNGE TUNDU LISSU AVULIWA UBUNGE, SABABU HIZI HAPA MBUNGE TUNDU LISSU AVULIWA UBUNGE, SABABU HIZI HAPA Reviewed by By News Reporter on 6/29/2019 07:53:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.