Loading...

LISSU AFANYIWA OPERESHENI YA 19, AWEKEWA CHUMA KATIKA MGUU WAKE

Loading...
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amewekewa chuma katika mguu wake wa kulia ili kuimarisha mfupa wa paja, ikiwa ni operesheni yake ya 19.

Rais huyo wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) juzi Machi 14, 2018 alifanyiwa upasuaji wa mguu wa kulia kama alivyoshauriwa na madaktari wa Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven, Gasthuisberg nchini Ubelgiji.

Akizungumza jana na Mwananchi Machi 15, 2018, Lissu amesema operesheni hiyo iliyochukua saa mbili ilifanywa na timu ya madaktari bingwa chini ya uongozi wa Profesa Willem-Jan Mertsemakers.

“Operesheni ilienda vizuri na kwa sasa naendelea na dawa na mapumziko hospitalini kwa muda wa angalau wiki tatu zinazokuja,” amesema Lissu.

 “Wameniwekea chuma cha kuimarisha mfupa wote wa paja la kulia. Pia wamechukua vipimo ili kuangalia kama hakuna tatizo la bacteria kabla hawajafunga kabisa sehemu ya kwenye goti ambayo haijaunga hadi sasa.”

Mke wa Lissu, Alicia amesema anamshukuru Mungu kwamba upasuaji huo umekwenda vyema.


Tuma neno 'HABARI' kwenda +255765112259 kupata habari za kitaifa punde zinapojiri.
LISSU AFANYIWA OPERESHENI YA 19, AWEKEWA CHUMA KATIKA MGUU WAKE LISSU AFANYIWA OPERESHENI YA 19, AWEKEWA CHUMA KATIKA MGUU WAKE Reviewed by By News Reporter on 3/16/2018 06:37:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.