Loading...

FAIZA ALLY AMWITA MTOTO WA MOBETO FEKI

Loading...
Mwanadada asiyeisha drama katika mitandao ya kijamii Faiza Ally amefunguka na kumjibu shabiki aliyetoa maoni ya kumshauri Faiza Ally hakumremba mtoto wake kama wanavyofanya wasanii wengine, lakini kitu cha ajabu wakati wa kumjibu shabiki Faiza Ally aliongea wazi kuwa hawezi kufanya hivyo kama anavyofanya Hamisa kwa watoto wake.

Katika maoni aliyoamua kujibu shabiki, faiza alisema kuwa hawezi kum-edit mtoto wake kama anavyofanya hamisa kwa mtoto wake na kumvalisha mawigi kwa sababu mtoto wake hivyo ndivyo alivyo.

"Siwezi kum-edit mtoto wangu mpaka apoteze uhalisia kama huyo wa mobeto , we are comfortable for who we are , na hizo nywele ndio asili yake ya uafrika , siwezi kumuweka dawa wala kumpachika viwigi …she born to be a star , she doesnt have to fake it , tunaishi maisha yetu kabisa."

Haijulikani kama kuna chochoko yoyote kati ya Hamisa na Faiza Ally mpaka afikie hatua ya kumuandikia hivi kuhusu mtoto wake.
Na Neema Joshua.




Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
FAIZA ALLY AMWITA MTOTO WA MOBETO FEKI FAIZA ALLY AMWITA MTOTO WA MOBETO FEKI Reviewed by By News Reporter on 5/29/2018 01:09:00 PM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.