Loading...

MKAPA, MBEKI KUTIKISA MDAHALO WA ELIMU UDOM

Loading...
Katika kuadhimisha miaka 10  tangu kuanzishwa kwake,  Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM),  kimeandaa mdahalo wa wanataaluma huku Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki akialikuwa kuwa mgeni rasmi.

Mada kuu katika mdahalo huo utakaofanyika Mei 18, 2018  na kuwahusisha wanataaluma kutoka vyuo vikuu mbalimbali nchini pamoja na viongozi wastaafu  na walioko madarakani ni hali ya elimu katika Afrika.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Jumamosi Mei 12, 2018 mjini Dodoma, Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Egid Mubofu amesema mhadhara huo ni mwanzo  wa mihadhara itakayokuwa inafanyika kila mwaka chuoni hapo kwa ajili ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere.

Amesema chuo hicho kitakuwa kinafanya mihadhara mbalimbali ya kitaaluma.

Amesema Mbeki ataambatana na mkuu wa chuo hicho, Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ambaye siku za hivi karibuni alipendekeza kufanyika kwa mdahalo wa kitaifa kujadili sekta ya elimu  nchini.
Na Fatma Pembe.



Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
MKAPA, MBEKI KUTIKISA MDAHALO WA ELIMU UDOM MKAPA, MBEKI KUTIKISA MDAHALO WA ELIMU UDOM Reviewed by By News Reporter on 5/13/2018 09:20:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.