Loading...
Watu zaidi ya 100 wamefariki dunia baada ya ndege ya kuwabeba abiria aina ya Boeing 737 kuanguka na kulipuka karibu na uwanja mkuu wa ndege wa Cuba mjini Havana, katika mkasa mbaya zaidi wa ndege nchini humo katika miongo kadha.
Wanawake watatu waliondolewa kutoka kwenye mabaki ya ndege hiyo wakiwa hai, lakini taarifa zinasema wamo hali mahututi.
Ndege hiyo, ambaye iliundwa karibu miaka 40 iliyopita, ilikuwa imewabeba abiria 104 na wahudumu sita wa ndege.
Serikali ya Cuba imeanzisha uchunguzi, na kutangaza siku mbili za maombolezo ya kitaifa.
Ndege hiyo Boeing 737-201 ilianguka saa sita na dakika nane mchana Ijumaa, muda mfupi baada ya kupaa kutoka Havana.
Ndege hiyo ilikuwa kwenye safari ya ndani ya nchi kutoka Havana kwenda Holguin, mashariki mwa Cuba.
Wahudumu wote sita wa ndege hiyo walikuwa raia wa Mexico lakini wengi wa abiria ni raia wa Cuba.
Na Hamisi Fakhi.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
Wanawake watatu waliondolewa kutoka kwenye mabaki ya ndege hiyo wakiwa hai, lakini taarifa zinasema wamo hali mahututi.
Ndege hiyo, ambaye iliundwa karibu miaka 40 iliyopita, ilikuwa imewabeba abiria 104 na wahudumu sita wa ndege.
Serikali ya Cuba imeanzisha uchunguzi, na kutangaza siku mbili za maombolezo ya kitaifa.
Ndege hiyo Boeing 737-201 ilianguka saa sita na dakika nane mchana Ijumaa, muda mfupi baada ya kupaa kutoka Havana.
Ndege hiyo ilikuwa kwenye safari ya ndani ya nchi kutoka Havana kwenda Holguin, mashariki mwa Cuba.
Wahudumu wote sita wa ndege hiyo walikuwa raia wa Mexico lakini wengi wa abiria ni raia wa Cuba.
Na Hamisi Fakhi.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
WATU ZAIDI YA 100 WAFARIKI BAADA YA NDEGE KUANGUKA CUBA
Reviewed by By News Reporter
on
5/19/2018 01:59:00 PM
Rating:

Hakuna maoni: