Loading...

MREMBO AANDIKA CV MTANDAONI ILI KUTAFUTA MCHUMBA

Loading...
Binti mmoja aliamua kuandika CV yake kuwavutia wanaume ili aweze kupata mchumba. Jumamosi Juni 2 katika mtandao wa Twitter aliandika wasifu wake wa kupendeza kwa lengo la kupata mchumba.

Msichana huyo, kwa jina Ogoo (@agochukjennifer) katika mtandao wa Twitter, alieleza kuwa anaweza kupika vizuri, ni mchapakazi kazini, ni mzuri na mwenye umbo la kuvutia.
Ogoo aliwaomba wafuasi wake kusambaza ujumbe huo kwa sababu inawezekana mchumba wake yupo katika kurasa zao.

Aliandika kupitia mtandao wa wakijamii, "Twitter fanya jambo. ninahitaji mpenzi, ninaweza kupika, ninafanya kazi, mimi ni mrembo na nina umbo la kuvutia. Naomba mueneze, labda mpenzi wangu yumo katika kurasa zenu. Na mimi sio bintiye Chimamanda. Asanteni," aliandika.
Na Neema Joshua.




Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
MREMBO AANDIKA CV MTANDAONI ILI KUTAFUTA MCHUMBA MREMBO AANDIKA CV MTANDAONI ILI KUTAFUTA MCHUMBA Reviewed by By News Reporter on 6/08/2018 07:24:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.