Loading...

WEMA AREJEA NCHINI BAADA YA MATIBABU YA NCHINI INDIA

Loading...
Mwana dada aliyewahi kuwa miss tanzania mwaka 2006 wema sepetu ameripotiwa kurudi kutoka india alipokwenda kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji na matatizo yanayomsumbua kwa muda sasa.

wema amnae aliripotiwa  wiki chache zilizopita mahakamani alipotakiwa kwenda kusikiliza kesi yake ya madawa ya kulevya ndipo mama yake aliposema kuwa mwana dada huyo alishindwa kufika kutokana na kupata safari ya ghafla  ya kwenda nje kwa matatibabu.

Alipokuwa akiongea na waandishi wa habari, meneja wa Wema Martin Kadinda amesema kuwa wema amereja kutoka india lakini hawezi kuongea mambo mengi kwa sasa kutokana na kuwa bado hayupo vizuri.

"Wema amerejea lakini kwa sasa hawezi kuzungumza  kwenye simu,anahitaji kupumzika kwa sababu amefanyiwa upasuaji ila anaendelea vizuri.

"Ninachoweza kukwambia ni upasuaji mdogo na ndio maana alikwenda peke yake,ninatumia nafasi hii kuwajulisha kuwa wema anaendelea vizuri."
NA Neema Joshua.




Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
WEMA AREJEA NCHINI BAADA YA MATIBABU YA NCHINI INDIA WEMA AREJEA NCHINI BAADA YA MATIBABU YA NCHINI INDIA Reviewed by By News Reporter on 6/08/2018 06:03:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.