Loading...

MREMA: DIAMOND MUZIKI WAKE UNAKOSHA ROHO, HATA KWA SISI WAZEE

Loading...
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Augustino Mrema amesema msanii wa Bongo Flava anayemfuatilia kwa sana ni Diamond Platnumz.

Ameeleza sababu ya kumfuatilia muimbaji huyo ni kutokana na kujituma kwake na muziki wake unavutia.

“Namfuatilia sana Diamond, ni kijana mdogo, muimbaji mahiri, yaani Diamond asaidiwe naona hatima yake katika maisha yake na nchi yetu atatufikisha mahali pazuri. Kwa muziki wake unakosha roho, hata sisi wazee, mimi naridhika sana,” Mrema ameiambia Times FM.

Katika hatua nyingine ametoa wito kwa serikali kuwa karibu zaidi na wasanii, hata hivyo amesema anaziona jitihada za Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe za kukutana na wasanii kila mara hasa pale wanapopata matatizo na kuwasaidia.
Na Peter Godwin.




Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
MREMA: DIAMOND MUZIKI WAKE UNAKOSHA ROHO, HATA KWA SISI WAZEE MREMA: DIAMOND MUZIKI WAKE UNAKOSHA ROHO, HATA KWA SISI WAZEE Reviewed by By News Reporter on 6/08/2018 06:25:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.