Loading...

SKENDO ZA UALAJI WA RAMBI RAMBI ZAMNG'ATUA STEVE KATIKA UONGOZI

Loading...
MSANII maaru­fu wa vichekesho Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amesema amekoma kuwa kiongozi misibani kwa sababu ya matusi anayovuna akishika nafasi hiyo.

Steve aliyasema hayo wikiendi iliyopita alipozungumza na mtandao mmoja wa habari hapa nchini, amekuwa akijitoa kwenye misiba ya wasanii wenzake lakini licha ya wema wake huo amekuwa akivuna skendo za ajabuajabu (kama ulaji fedha za rambirambi) na matusi jambo ambalo linamhuzunisha na kuiathiri familia yake.

“Unajua mimi nina wa­toto, sasa wanapoona ya­nayoandikwa mitandaoni ya kunitukana na kunifedhehesha kwa vitu vya uongo wa­tanichukuliaje, niseme tu huu msiba wa mtoto Patrick Peter ambaye ni mtoto wa msanii mwenzangu Muna ndiyo wa mwisho, sitajihusisha tena na uongozi; kwenye misiba nita­shiriki kama mtu wa kawaida,” alisema Steve.

Kwa sasa Steve ameona bora kubwaga manyanga Skendo zitamshushia hadhi japo lengo lake lilikuwa zuri.
Na Catherine Kisese.




Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
SKENDO ZA UALAJI WA RAMBI RAMBI ZAMNG'ATUA STEVE KATIKA UONGOZI SKENDO ZA UALAJI WA RAMBI RAMBI ZAMNG'ATUA STEVE KATIKA UONGOZI Reviewed by By News Reporter on 7/11/2018 12:23:00 PM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.