Loading...
Aliyekuwa kiongozi wa kundi la wanamgambo wa kiislamu nchini Somalia, Alshababaab ametangaza kuwa anawania uongozi serikalini.
Mukhtaar Roobow anayefahamika pia kama Abu Mansur, alijitoa katika kundi la Alshabaab mnamo 2012 lakini alijisalimisha kwa serikali ya Somalia mnamo Agosti mwaka jana.
Atawania urais wa jimbo la ksuini magharibi mwa Somalia katika uchaguzi wa kieneo mwezi ujao.
Mukhtar Robow amesema uamuzi huo kuingia katika siasa ni kufuatia wito wa wananchi, wafuasi wake katika jimbo hilo la kusini magharibi.
Amedhihirisha kwamba yupo tayari iwapo atashinda, kuidhinisha uhusiano thabiti na serikali ya shirikisho katika mji mkuu Mogadishu, ambayo imekuwa katika mzozo na tawala za baadhi ya majimbo.
Mukhtaar Roobow ni kiongozi wa juu zaidi katika kundi la al-Shabab kuwahi kujitoa kutoka kundi hilo na kujisalimisha, licha ya kuwa mojawapo ya waasisi wa kundi hilo.
Na Yahya Juma.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
Mukhtaar Roobow anayefahamika pia kama Abu Mansur, alijitoa katika kundi la Alshabaab mnamo 2012 lakini alijisalimisha kwa serikali ya Somalia mnamo Agosti mwaka jana.
Atawania urais wa jimbo la ksuini magharibi mwa Somalia katika uchaguzi wa kieneo mwezi ujao.
Mukhtar Robow amesema uamuzi huo kuingia katika siasa ni kufuatia wito wa wananchi, wafuasi wake katika jimbo hilo la kusini magharibi.
Amedhihirisha kwamba yupo tayari iwapo atashinda, kuidhinisha uhusiano thabiti na serikali ya shirikisho katika mji mkuu Mogadishu, ambayo imekuwa katika mzozo na tawala za baadhi ya majimbo.
Mukhtaar Roobow ni kiongozi wa juu zaidi katika kundi la al-Shabab kuwahi kujitoa kutoka kundi hilo na kujisalimisha, licha ya kuwa mojawapo ya waasisi wa kundi hilo.
Na Yahya Juma.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
KIONGOZI WA ALSHABAAB AJITOSA KATIKA SAKATA LA MBIO ZA URAIS
Reviewed by By News Reporter
on
10/05/2018 07:25:00 AM
Rating:

Hakuna maoni: