Loading...
Cuba imeadhimisha miaka 60 ya mapinduzi ya taifa hilo dhidi ya aliyekuwa mtawala wa kiimla, Fulgencio Batista, huku kiongozi wa chama tawala cha kikomunisti, Raul Castro, akiwaasa Wacuba kuendelea kuilinda misingi ya mfumo wa kijamaa licha ya changamoto za kilimwengu na kikanda.
Kwenye hotuba yake ya maadhimisho hayo, Raul Castro - ambaye kwa sasa ni rais mstaafu na pia mwenyekiti wa chama tawala - ameituhumu vikali serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani, kwa kurejea kwenye mipango yake ya kizamani ya kukabiliana na taifa hilo pamoja na uingiliaji wake kwenye eneo la Amerika ya Kusini.
"Kwa kuwa malengo ya kibeberu yamerejeshwa katika ukanda wetu, Wamarekani wanapaswa kuelewa kuwa Amerika ya Kusini na Caribbean zimebadilika, lakini pia ulimwengu. Sisi tutaendelea kushinikiza kikamilifu mchakato wa makubaliano na ushirikiano wa kanda, kulingana na dhana ya umoja katika utangamano." alisema Castro kwenye sehemu ya hotuba yake.
Katika Siku ya Mwaka Mpya ya mwaka 1959, jeshi la kimapinduzi chini ya uongozi wa Fidel Castro pamoja na ndugu yake Raul walifanikiwa kuyaangusha majeshi ya serikali baada ya miaka miwili ya vita vya msituni, na hatimaye mtawala wa kiimla wakati huo, Fulgencio Batista, aliyekuwa akiungwa mkono na Marekani kukimbilia ughaibuni.
Na Khalid Juma.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
Kwenye hotuba yake ya maadhimisho hayo, Raul Castro - ambaye kwa sasa ni rais mstaafu na pia mwenyekiti wa chama tawala - ameituhumu vikali serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani, kwa kurejea kwenye mipango yake ya kizamani ya kukabiliana na taifa hilo pamoja na uingiliaji wake kwenye eneo la Amerika ya Kusini.
"Kwa kuwa malengo ya kibeberu yamerejeshwa katika ukanda wetu, Wamarekani wanapaswa kuelewa kuwa Amerika ya Kusini na Caribbean zimebadilika, lakini pia ulimwengu. Sisi tutaendelea kushinikiza kikamilifu mchakato wa makubaliano na ushirikiano wa kanda, kulingana na dhana ya umoja katika utangamano." alisema Castro kwenye sehemu ya hotuba yake.
Katika Siku ya Mwaka Mpya ya mwaka 1959, jeshi la kimapinduzi chini ya uongozi wa Fidel Castro pamoja na ndugu yake Raul walifanikiwa kuyaangusha majeshi ya serikali baada ya miaka miwili ya vita vya msituni, na hatimaye mtawala wa kiimla wakati huo, Fulgencio Batista, aliyekuwa akiungwa mkono na Marekani kukimbilia ughaibuni.
Na Khalid Juma.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
CUBA YAADHIMISHA MIAKA 60 YA MAPINDUZI
Reviewed by By News Reporter
on
1/03/2019 09:12:00 AM
Rating:

Hakuna maoni: