Loading...

MAMA ALIYEVUMILIA MIAKA 18 KATIKA NDOA BILA MTOTO, AJIFUNGUA MAPACHA 5

Loading...
Mwanamke mwenye umri wa miaka 42 amejifungua watoto watano Katika Kituo cha Afya cha Federal Medical (FMC) Lokoja, Nigeria baada ya miaka 18 ya kusubiri.

Okeigbo alijifungua salama wavulana watatu na wasichana wawili Jumatano, Aprili 17, kupitia njia ya upasuaji.

Akihojiwa na NAN, mwanamke huyo alimshukuru Mungu kwa zawadi hiyo adimu huku akimmiminia sifa tele mume wake kwa kuwa naye kipindi chote cha ujauzito. 

“Si rahisi kupata watoto watano kwa wakati mmoja,” alisema. 

Mara baada ya kuzaliwa, wavulana walikuwa na uzani wa 1.3kg 1.6kg, 1.7kg, na wasichana 1.8kg na 1.9kg, mtawalia.

Baba wa watoto hao James Okeigbo, 47, alikuwa na furaha tele na kusema tukio hilo atalikumbuka maishani na limempa yeye na mke wake amani moyoni. 

”Namshukuru mke wangu kwa kuwa mwaminifu kwangu kwa kipindi chote cha miaka 18 tulipokuwa hatuna mtoto. Pia anashukuru familia yake kwa kusimama nasi," alisema. 

Hata hivyo, James aliiomba serikali na umma kumsaidia kuwalea watoto hao kwa kuwa yeye binafsi anahisi hatoweza.

Grace Ogoke, ambaye ni daktari aliyemzalisha mama huyo alisema ni furaha tele kwa mama huyo kujifungua salama hata ingawa alijifungua kupitia njia ya upasuaji. 

Kulingana na daktari, wazazi hao walikuja katika hospitali hiyo kutafuta huduma na walikuwa na matatizo ya kupata watoto. 

Lakini baada ya hospitali hiyo kuchukua jukumu, madaktari walifanya utafiti na kisha wakamwezesha mama kupata mimba na wakailea hadi alipowazaa watoto hao watano.

Daktari mkuu katika FMC, Olatunde Alabi, alisema tukio hilo lilikuwa la kwanza kuwahi kutokea katika hospitali hiyo na kwamba wote waliohusika katika kumzalisha mama huyo ni nguli wa kazi. 

"Najisikia vizuri sana na namshukuru Mungu kwa kutuwezesha, kwa kuwa nahisi ni kama sote tulikuwa wajawazito wakati wa ujauzito wake huo. Idadi kubwa ya watoto tuliopata mama akijifungua ni watatu lakini hii ni mara ya kwanza tumepata watano," Alabi alisema.
Na Neema Joshua.
.
.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
MAMA ALIYEVUMILIA MIAKA 18 KATIKA NDOA BILA MTOTO, AJIFUNGUA MAPACHA 5 MAMA ALIYEVUMILIA MIAKA 18 KATIKA NDOA BILA MTOTO, AJIFUNGUA MAPACHA 5 Reviewed by By News Reporter on 4/21/2019 09:22:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.