Loading...

WAANDAMANAJI WA VIZIBAO VYA NJANO WAANZA UPYA NCHINI UFARANSA

Loading...
Waandamanaji wa vizibao vya njano wameanza upya kuandamana dhidi ya utawala wa Macron nchini Ufaransa.

Maandamano ya vizibao vya njano, ambayo yalianza kwa nia ya kukabiliana na kuongezeka kwa mafuta na hali mbaya za kiuchumi na kisha yakageuka kuwa maandamano dhidi ya utawala wa Macron, yanaendelea kwa wiki ya 23 sasa.

Mjini Paris, kulikuwa na mvutano kati ya waandamanaji na polisi, ambao walitembea kutoka Bataillon du Pacifique Square hadi Republique Square.

Polisi waliingilia kati wanaharakati ambao walikuwa wakitumia chupa na mawe kwa kuwashambulia na mabomu ya machozi.

Watu 227 wametiwa chini ya ulizni huku wengine 5,518 wakiwa wamechunguzwa vibali vyao nchini humo.

Watu elfu 27,900 wameshiriki katika maandamano hayo.

Maandamano yamefanyika katika miji kama vile Bordeaux, Marseille na Montpellier.

Polisi elfu 60 wametumikia katika maandamano nchini kote. Usafiri wa metro umesimamishwa mjini Paris imesimama.

Maandamano ya vizibao vya njano  yameendelea tangu Novemba 17, 2018.

Kulingana na takwimu za serikali, watu 11 wamepoteza maisha yao na zaidi ya watu 2,000 wamejeruhiwa. Zaidi ya watu elfu 8 wametiwa kizuizini na karibu watu elfu wamefungwa.
Na Baraka Amani.
.
.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
WAANDAMANAJI WA VIZIBAO VYA NJANO WAANZA UPYA NCHINI UFARANSA WAANDAMANAJI WA VIZIBAO VYA NJANO WAANZA UPYA NCHINI UFARANSA Reviewed by By News Reporter on 4/21/2019 03:26:00 PM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.