Loading...

ATUPWA JELA KWA KUPANDA BANGI KANISANI

Loading...
Jamaa mmoja alifungwa jela baada ya kupatikana na hatia ya kupanda mmea wa bangi katika shamba la Kanisa Katoliki katika dayosisi ya Eldoret.

Joash Kipchirchir ambaye alikuwa akifanya kazi katika shamba hilo alifikishwa katika mahakama ya Eldoret na kupatikana na hatia ya kupanda bangi katika shamba hilo la kanisa.

Kulingana na kisa hicho kilichochapishwa katika gazeti moja huko nchini Kenya, Kipchirchir alikiri makosa yake mbele ya hakimu Mkuu wa Eldoret.

Kipchirchir alijiteteta akieleza kuwa alijua alikuwa amepanda maua wala si mmea wa bangi na akamuomba hakimu huyo kumsamehe.

Akitoa hukumu, hakimu huyo alieleza kuwa kosa hilo lilihitaji kifungo cha miaka mitano au faini ya KSh 250 lakini akumuonea huruma mshatakiwa na kumpa kifungo cha miezi sita ama faini ya KSh 50,000.
Na Catherine Kisese.




Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
ATUPWA JELA KWA KUPANDA BANGI KANISANI ATUPWA JELA KWA KUPANDA BANGI KANISANI Reviewed by By News Reporter on 6/13/2018 09:45:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.