Loading...

BILIONEA DANGOTE ASAKA MKE WA KUOA

Loading...
Ushawi kuwahi kuota kuolewa na mtu mwenye pesa chafu?. Kwa sasa Aliko Dangote, mtu tajiri barani Afrika amefunguka na kusema kwa sasa ana umri wa miaka 61, lakini yupo tayari kuoa mke mpya.

Fikiria, kama jamaa yako akuridhishi kwa kipata hebu tafuta namna ya kujipenyeza katika njia ya Dangote unaweza kutoboa kama wanavyosema vijana wa kileo.

Akizungumza na David Piling katika mahojiano na jarida la Fanancial Times, Bilionea huyo ameweka wazo upande wake wa kimahusiano.

Dangote alifunguka kwamba ratiba zake zinakinzana na maisha ya kimapenzi. Mwanzilishi wa Dangote Group, ambaye ameachika zaidi ya mara moja na mwenye watoto wakubwa wa kike, ameiambia jarida hilo kwamba yupo mbioni kufunga ndoa nyingine.

Kutokana na mahojiano hayo na kwakuweka wazi nia yake hiyo mpaka sasa taarifa zilizopo chini ya kapeti ni kuwa wameshajitokeza wanawake zaidi ya 800 wanaotaka kuolewa na Dangote.
Na Paskali Joseph.




Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
BILIONEA DANGOTE ASAKA MKE WA KUOA BILIONEA DANGOTE ASAKA MKE WA KUOA Reviewed by By News Reporter on 7/14/2018 05:33:00 PM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.