Loading...

MFUNGWA SUGU ATOROKA MAGEREZA KWA KUTUMIA HELIKOPTA NCHINI UFARANSA

Loading...
Rédoine Faïd, ni mfungwa sugu ambae anafahamika vema katika ofisi za magereza nchini Ufaransa. Mfungwa huyo kwa mara nyingine ametoroka magaereza kwa kutumia  helikopta Jumapili majira ya asubuhi.

Taarifa kuhusu kutoroka kwa mfungwa huyo imetolewa na vyomba vya habari nchini Ufaransa. 

Kulingana na taarifa zilizotolewa na Francetvinfo, Redoine Faid  ametoroka kutoka katika gereza la Reau Seine-et-Marne  akisaidiwa na wahalifu wenzake wanne waliowasili na helikopta hiyo walikiwa awamejihami na silaha. 

Wahalifu hao baada ya kuwasili katika gereza hilo walivunja milango kwa lengo la kumtorosha Faid. 

Hakuna mtu yeyote aliejeruhiwa  katika operesheni hiyo ya kihalifu ilioendeshwa kwa muda wa dakika chache.

Helikopta iliotumiwa kumtorosha Faid ilikutwa ikiwa imechomwa moto  karibu na uwanja wa ndege wa Roissy mjini Paris.

Faid alihukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka 25 gerezani.
Na Geofrey Okechi.



Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
MFUNGWA SUGU ATOROKA MAGEREZA KWA KUTUMIA HELIKOPTA NCHINI UFARANSA MFUNGWA SUGU ATOROKA MAGEREZA KWA KUTUMIA HELIKOPTA NCHINI UFARANSA Reviewed by By News Reporter on 7/03/2018 11:16:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.