Loading...
Kila mmoja wetu ana uwezo mkubwa wa ubunifu ndani yake ambao siku zote upo unasubiri uweze kutumika. Watu wengi hatutambui hili na tumekuwa tukifiri kama uwezo huu uko kwa baadhi ya watu fulani tu na kwamba wengine hawana.
Ili kuweka sawa mtazamo huu, tofauti pekee iliyopo ni kwamba watu wanaoonesha uwezo mkubwa wa ubunifu huwa kuna kitu ambacho kinawasukumu na kuwalazimisha kuwa wabunifu.
Kwa kawaida mawazo ya ubunifu hujitokeza pale unapokuwa na lengo fulani unataka kulifanikisha. Kukosekana kwa lengo madhubuti linalosumbua akili kulifanikisha kamwe huwezi kuwa mbunifu.
Jaribu kujiwekea malengo fulani na pia nia ya dhati ya kutaka kuyafanikisha na utashuhudia ubunifu mkubwa ulioko ndani yako. Wengi tunaishi maisha yetu yote na kuiacha hazina kubwa ya ubunifu iliyo ndani yetu bila kutumika.
Keep Moving Forward!
Vicent Stephen
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
'MAWAZO YA UBUNIFU HUJITOKEZA PALE UNAPOKUWA NA LENGO FULANI UNATAKA KULIFANIKISHA'
Reviewed by By News Reporter
on
8/26/2018 12:54:00 PM
Rating:
Hakuna maoni: