Loading...

MUZIKI WA DANSI WAFANYA KWELI KATIKA ONYESHO LA TüBINGEN,UJERUMANI

Loading...
Ilikuwa katika viwanja vya maonyesho ya International Afrika Festival Tübingen nchini ujerumani ambapo katika maonyesho hayo mwaka huu 2018 nchi lengwa ilikuwa ni Tanzania na mgeni wa heshima rasmi alikuwa balozi wa Tanzania nchini ujerumani mheshimiwa Dkt. Abdallah Possi ambaye alihutubia ummati wa kadamnasi ya waudhuriaji wakiwemo wawekezaji kuwa Tanzania kuna fursa kubwa za uwekezaji na pia nchi salama.

Onyesho hilo kubwa lilinogeshwa na bendi za muziki kama Ngoma Africa band maarufu FFU-Ughaibuni inayoongozwa na kamanda Ras Makunja, bendi ya Mvula-Mandondo Band inayoongozwa na msanii Saidi Kanda yenye maskani kule Uingereza nayo ilifanya vizuri,wasanii wa kizazi kipya kama Nashi MC kutoka Tanzania naye alitingisha jukwaa msanii wa picha za kuchora Chilonga Haji naye alikuwa moja ya waonyeshaji wa bidhaa toka Tanzania.

Onyesho lilifana sana sana na kuitanga za Tanzania kimataifa.
Na Hamisa Geofrey.




Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
MUZIKI WA DANSI WAFANYA KWELI KATIKA ONYESHO LA TüBINGEN,UJERUMANI MUZIKI WA DANSI WAFANYA KWELI KATIKA ONYESHO LA TüBINGEN,UJERUMANI Reviewed by By News Reporter on 8/17/2018 04:49:00 PM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.