Loading...

VISA NA MIKASA: MWANAMKE ATIMUA MBIO KWA MGANGA KWA HOFU YA KUGEUZWA BATA

Loading...
Mwanamke mmoja wa mtaa wa Kivumbini, Nakuru - Kenya alilazimika kutimuka mbio baada ya kushindwa kutimiza kanuni za mganga.

Hii ni baada ya kufika kwa mganga huyo akitaka mganga amthibitishie kama kweli mumewe alikuwa akimpenda kwa dhati.

Mganga alikataa kumpa dawa na kumdai malipo ya mbuzi watano. Mwanamke huyo ambaye hakuwa na uwezo wa kulipa alitaka kupewa dawa kwanza kabla kulipa.

''Sisi hapa hatubahatishi, leta mbuzi watano nikuonyeshe maajabu ama nikubadilishe uwe bata saa hii,’’ mganga alimtishia mama huyo. 

Kwa woga alitimka mbio akiapa kutoshiriki ushirikina tena.
Na Neema Joshua.




Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com au sms-whatsapp: +255765112259
VISA NA MIKASA: MWANAMKE ATIMUA MBIO KWA MGANGA KWA HOFU YA KUGEUZWA BATA VISA NA MIKASA: MWANAMKE ATIMUA MBIO KWA MGANGA KWA HOFU YA KUGEUZWA BATA Reviewed by By News Reporter on 8/23/2018 08:35:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.