Loading...
Kapteni wa zamani wa Manchester United, Wayne Rooney amesema kuwa tatizo la timu hiyo siyo kocha Jose Mourinho bali wachezaji.
Rooney aliondoka United akaenda Everton na msimu huu anaitumikia DC United ya Ligi Kuu ya Marekani, MLS.
Rooney ambaye ana aminika kuwa ni mchezaji makini sana, amesema kuwa wachezaji wa timu hiyo wanatakiwa kujitazama upya na kuanza kuipambania timu hiyo na siyo kuacha lawama zote kwa kocha Jose Mourinho.
Rooney amesema kama wachezaji hao wataonyesha kiwango chao basi United inaweza kupata matokeo mazuri uwanjani.
Manchester United wamekuwa na matokeo mabaya kwa siku za hivi karibuni na sasa wapo katika nafasi ya nane wakiwa na pointi 13 tu wakiwa wameshacheza michezo nane.
Wikiendi iliyopita timu hiyo ilipata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Newcastle United, ukiwa ni wa kwanza kwao kuanzia Septemba 19.
Na Khalid Juma.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com
Rooney aliondoka United akaenda Everton na msimu huu anaitumikia DC United ya Ligi Kuu ya Marekani, MLS.
Rooney ambaye ana aminika kuwa ni mchezaji makini sana, amesema kuwa wachezaji wa timu hiyo wanatakiwa kujitazama upya na kuanza kuipambania timu hiyo na siyo kuacha lawama zote kwa kocha Jose Mourinho.
Rooney amesema kama wachezaji hao wataonyesha kiwango chao basi United inaweza kupata matokeo mazuri uwanjani.
Manchester United wamekuwa na matokeo mabaya kwa siku za hivi karibuni na sasa wapo katika nafasi ya nane wakiwa na pointi 13 tu wakiwa wameshacheza michezo nane.
Wikiendi iliyopita timu hiyo ilipata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Newcastle United, ukiwa ni wa kwanza kwao kuanzia Septemba 19.
Na Khalid Juma.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com
ROONEY AWAPA MAKAVU MAN UTD
Reviewed by By News Reporter
on
10/11/2018 06:52:00 AM
Rating:
Hakuna maoni: