Loading...
Mamia ya wafuasi wa mgombea huyo waliokuwa wakiongozana kumlaki kiongozi wao wametawanywa kwa mabomu ya machozi na kurushiwa maji ya moto karibu na sehemu ya kuegesha magari kwenye uwanja wa ndege, kwa mujibu wa mwandishi wa habari wa AFP.
Magari kumi ya polisi na malori kadhaa ya kikosi cha kutuliza ghasia yamekuwa yameegesha karibu na uwanja wa ndege wa Lubumbashi, mji wa pili wa DRC na mji mkuu wa nchi hiyo kwa madini ambao unapiganiwa na utawala na upinzani.
Hata hivyo Martin Fayulu amewasili katika uwanja wa ndege wa Lubumbashi na kuondoka akiwa ndani ya gari ndogo, huku msafara wake ukiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi hadi katikati ya mji ambako anatarajia kuendesha kampeni yake.
Mmoja wa wanasiasa wakuu wanaomuunga mkono ni gavana wa zamani wa Katanga na mtu maarufu Lubumbashi, Moise Katumbi, aliye uhamishoni nchini Ubelgiji.
Lubumbashi pia ni ngome ya rais wa sasa, Joseph Kabila, ambapo "mgombea wake", Emmanuel Ramazani Shadary, alianza kampeni yake Novemba 26.
Upinzani umegawanyika kati ya Bw Fayulu na Felix Tshisekedi, mgombea wa chama cha kihistoria cha UDPS, ambaye alitoa saini yake kwenye mkataba wa Geneva kuhusu uteuzi wa mgombea mmoja, saa 24 baada ya kutia saini.
Na Mussa Hamisi.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
Magari kumi ya polisi na malori kadhaa ya kikosi cha kutuliza ghasia yamekuwa yameegesha karibu na uwanja wa ndege wa Lubumbashi, mji wa pili wa DRC na mji mkuu wa nchi hiyo kwa madini ambao unapiganiwa na utawala na upinzani.
Hata hivyo Martin Fayulu amewasili katika uwanja wa ndege wa Lubumbashi na kuondoka akiwa ndani ya gari ndogo, huku msafara wake ukiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi hadi katikati ya mji ambako anatarajia kuendesha kampeni yake.
Mmoja wa wanasiasa wakuu wanaomuunga mkono ni gavana wa zamani wa Katanga na mtu maarufu Lubumbashi, Moise Katumbi, aliye uhamishoni nchini Ubelgiji.
Lubumbashi pia ni ngome ya rais wa sasa, Joseph Kabila, ambapo "mgombea wake", Emmanuel Ramazani Shadary, alianza kampeni yake Novemba 26.
Upinzani umegawanyika kati ya Bw Fayulu na Felix Tshisekedi, mgombea wa chama cha kihistoria cha UDPS, ambaye alitoa saini yake kwenye mkataba wa Geneva kuhusu uteuzi wa mgombea mmoja, saa 24 baada ya kutia saini.
Na Mussa Hamisi.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
UCHAGUZI CONGO: WAFUASI WA MGOMBEA WA UPINZANI FAYULU WASAMBARATISHWA LUBUMBASHI
Reviewed by GEOFREY MASHEL
on
12/12/2018 10:29:00 AM
Rating:
Reviewed by GEOFREY MASHEL
on
12/12/2018 10:29:00 AM
Rating:

Hakuna maoni: