Loading...
Wizara ya mambo ya ndani nchini Burundi yapiga marufuku kufunguliwa kwa nyumba za ibada mjini Bujumbura
Tangazo lililotolewa na wizara ya mambo ya ndani nchini Burundi limefahamisha kuwa ni marufuku mjini Bujumbura kufunguliwa kwa nyumba ya ibada bila ya mamlaka husika kupewa taarifa na kuruhusiwa na serikali.
Katika miaka ya hivi karibuni, makanisa ya uamsho mjini Bujumbura yameongezeka kwa kiasi kikubwa huku yakiwa hayatambuliki katika uongozi mkuu wa kanisa.
Idadi ya wakazi wa jiji la Bujumbura imeripotiwa kuzidi kuongeza kila mwaka na kufikia watu milioni 2.
Nchini Burundi, asilimia 80 ya raia wake ni wakristo huku asilimia 10 ikiwa ni waislamu na imani nyingine.
Viongozi wa dini hawajatoa tamko lolote kufaatia sheria hiyo.
Tangazo lililotolewa na wizara ya mambo ya ndani nchini Burundi limefahamisha kuwa ni marufuku mjini Bujumbura kufunguliwa kwa nyumba ya ibada bila ya mamlaka husika kupewa taarifa na kuruhusiwa na serikali.
Katika miaka ya hivi karibuni, makanisa ya uamsho mjini Bujumbura yameongezeka kwa kiasi kikubwa huku yakiwa hayatambuliki katika uongozi mkuu wa kanisa.
Idadi ya wakazi wa jiji la Bujumbura imeripotiwa kuzidi kuongeza kila mwaka na kufikia watu milioni 2.
Nchini Burundi, asilimia 80 ya raia wake ni wakristo huku asilimia 10 ikiwa ni waislamu na imani nyingine.
Viongozi wa dini hawajatoa tamko lolote kufaatia sheria hiyo.
Na Zakaria Bernard.
.
.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
BURUNDI YAPIGA MARUFUKU UJENZI WA NYUMBA ZA IBADA
Reviewed by By News Reporter
on
4/20/2019 08:19:00 AM
Rating:
Hakuna maoni: