Loading...
“Tuliamua Dk. Kimei apumzike na kumpisha Mkurugenzi Mtendaji mpya kwa kutilia maanani misingi ya utawala bora na maadili yetu ya kazi kuwa ingeleta ugumu kwa benki kuwa na wakurugenzi watendaji wawili kwa pamoja kwa kipindi kirefu. Kwetu sisi Nsekela ni kijana na askari wetu wa miamvuli anayerejea nyumbani, ni mtu makini na sahihi wa kuiongoza benki ya CRDB kuingia kwenye zama mpya zinazotilia mkazo mapinduzi ya teknolojia”. Ameeleza Mwenyekiti huyo.
Mwezi Desemba mwaka jana, Dk. Kimei alitangaza kustaafu wadhifa wake ndani ya benki hiyo baada ya kudumu katika uongozi kwa takribani miaka 20 ambapo alieleza kuwa aliamua kutoongeza mkataba kwa hiari na kwamba atabaki kuwa mwanahisa na mteja wa CRDB. Mkurugenzi Mtendaji mpya wa benki hiyo, Abdulmajid Nsekela, aliripoti ofisini tarehe 01 Oktoba na kukabidhiwa rasmi ofisi Oktoba 02 na kuanza kazi.
Na Hamisi Shamte.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
KILICHOMUONDOA MKURUGENZI MTENDAJI 'KIMEI' CRDB MAPEMA
Reviewed by By News Reporter
on
10/12/2018 07:53:00 AM
Rating:
Hakuna maoni: