Loading...

KOCHA MOURINHO AFUNGUKA SABABU YA KUFUKUZWA MAN UTD, POGBA AHUSISHWA

Loading...
Aliyekuwa kocha wa klabu ya Manchester United Jose Mourinho amesema kuwa matatizo yanayoisumbua klabu hiyo yanaanzia kwa wachezaji. 

Kocha huyo amefichua kuwa, mfumo na malengo ya klabu nzima vimechangia zaidi kuporomoka kwa klabu na kuongezea kutaja Paul Pogba kuwa chanzo cha kuachishwa kazi.

Mourinho ambaye alikuwa kocha mkuu wa Man United, alitimuliwa kazi mwezi Disemba, baada ya matatizo ya mahusiano kati yake na Pogba kuanza mwezi Septemba. 

Mgogoro huo ulimfanya kocha huyo kumpa unahodha kuweka mambo sawa ndani ya klabu na hata uwanjani ingawa haikuwa kama ilivyotarajiwa.

Akihojiwa na gazeti maarufu la michezo nchini Ufaransa L’Equipe , Mreno huyo alifunguka na kusema ni kweli Pogba alichangia kutimuliwa kwake. 

“Sio hivyo, matatizo yapo pale, unaweza kuamini kuwa matatizo ni wachezaji, mfumo na malengo.” alisema. 

Mourinho alipoulizwa ikiwa ni kweli anadhani Pogba ndiyo chanzo cha kutimuliwa Old Trafford, alikuwa mjanja wakati akijibu swali hilo.

“Nitaweza kusema tu kwamba, siwezi kusema ndio, uliponiuliza kama Paul Pogba ni yeye tu anayewajibika.” Mourinho alisema.

Baada ya kuondoka kwa mreno huyo, Ole Gunnar Solskjaer alichukuliwa kiziba pengo la Mourinho kwa kupewa mkataba wa miaka mitatu.

Kocha huyo mpya kwanza aliitumikia United kwa muda akiwa kocha wa muda na alishinda mechi 14 kati ya 19 mara baada ya kuanza kazi na hatimaye kuisaidia timu hiyo kurejea tano bora kwenye jedwali. 

Hata hivyo matokeo ya timu hayajakuwa ya kuridhisha hadi ligi inakamilika na huenda kazi inaanza kumshinda hasa baada ya kocha huyo kushindwa kuifanya Manchester United kumaliza miongoni mwa timu nne bora na badala yake kumaliza katika nafasi ya sita.
Na Shamimu Ally.
.
.
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri mkuu:dundiikaonline@gmail.com.
KOCHA MOURINHO AFUNGUKA SABABU YA KUFUKUZWA MAN UTD, POGBA AHUSISHWA KOCHA MOURINHO AFUNGUKA SABABU YA KUFUKUZWA MAN UTD, POGBA AHUSISHWA Reviewed by By News Reporter on 5/16/2019 09:34:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Loading...
Inaendeshwa na Blogger.