Loading...

ALICHOANDIKA MSEMAJI WA IKULU 'MSIGWA' JUU YA AFYA YA RUGE

Majuma Kadhaa hapo yaliyopita, Ndg. Ruge Mutahaba bosi wa Clouds Media Group alisafirshwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu akisumbuliwa na maradhi ya figo.

Ndugu, marafiki, jamaa na hata viongozi wa serik
Loading...
li akiwemo rais wetu Magufuli wametuma salamu za pole kwa kutoa kiasi cha Sh. milioni 50 ili zimsaidie Mtanzania mwenzetu katika matibabu yake.

Lakini msemaji wa Ikulu Gerson Msigwa naye hakuwa nyuma naye alituma salamu zake za pole na kumuombea kwa Mungu Ndg Ruge Mutahaba apate nafuu kwani bado tunampenda na kumuhitaji katika ujenzi wa taifa letu. Aliandika kupitia mtandao wa Instagram, alisema:

"Kama ambavyo umekuwa ukipigania maisha ya wengine na wakasimama nakuombea sana mapambano haya ya uhai wako ushinde kwa kishindo. Pole sana, nakuomba Mwenyezi Mungu shusha uponyaji kwa mtu huyu. Sote tumuombee Ndg yetu Ruge Mutahaba ayashinde maradhi yanayomkabili @cloudstv @cloudsfmtz."

Na Haika Gabriel.
ALICHOANDIKA MSEMAJI WA IKULU 'MSIGWA' JUU YA AFYA YA RUGE ALICHOANDIKA MSEMAJI WA IKULU 'MSIGWA' JUU YA AFYA YA RUGE Reviewed by By News Reporter on 11/27/2018 06:34:00 AM Rating: 5

Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.